📖 Vitabu vya Riwaya vya Waandishi Nguli Nchini Tanzania 🇹🇿
Wahuni Wote Peponi
NEW
Kitabu Digitali

Wahuni Wote Peponi

Maisha ya walimwengu yamejaa visa na mikasa ya kusisimua. Hata hivyo, katika miji na majiji wanawake na wanaume huishi kila mmoja na mtindo wake ili kukidhi mahitaji ya kila siku. Katika harakati za kuisaka riziki na kuiepa dhiki, hapa ndipo kudra na juhudi hujitokeza. Wapo wapatao mali na kuwa na maisha ya kustarehe na wapo ambao huishi kwa kuunga tumaini wakitegemea wenye nazo. Hapo ndipo kunazaliwa riwaya hii ya kusisimua, wahuni wote peponi. Tunakutana na Mwamba Mzeta na wahuni wenzake dhidi ya mdangaji aliyekubuhu, Sijali na mashogaze, akiwajumuisha Avijawa na Amina, hawa ni wenye kiu ya kuishi kwa jasho la waume ambao nao wanahitaji starehe ya faragha. Inakuwa kukomoana na kukomeshana. Japo mwandishi ameandika riwaya hii kwa wingi wa visa vya kuchekesha na lugha iliyojaa kejeli kutoka kwa wahusika, riwaya hii imeyaakisi maisha halisi ya wakazi wa jiji la Dar es salaam hasa TANDIKA, eneo la BUZA na maeneo mbalimbali ya jirani. Kutano la wahuni na wasaka riziki linazaa misukosuko ya maisha yanayopelekea vyombo vya dola kuwajibika kwa upande mmoja, lakini mwisho wa dhiki ni faraja. Kitabu hiki kitakufurahisha na kukufunza juu ya maisha ambayo hujawahi kuyawaza, kwani mengi hufanyika sirini lakini mwandishi amefanikiwa kuyaonesha kwa uwazi. Mwamba Mzeta ndiye aliyeasisi jina la kitabu hiki akiwa na wahuni wenzake kilingeni kwa kusema, “Wahuni wote peponi! Hatunaga unafiki— hiyo pekee inatuhusu!?

1 Faili
TZS 7,000
Angalia Maelezo
Sanda ya Jambazi
Kitabu Digitali

Sanda ya Jambazi

Riwaya hii, SANDA YA JAMBAZI, inaendeleza pale ilipoishia ile riwaya iliyowasisimua wengi, UKIMWONA MMALIZE! Inspekta Sindi na Koplo Fideli, ambae hivi karibuni amepandishwa cheo na kuwa Sajenti, ndio waliokuwa wakishughulikia upelelezi katika riwaya hiyo na kukutana nao tena katika riwaya hii. Jambazi linalohusika ni lile lile Malik Mbowe. Katika kulifukuza jambazi hilo, Inspekta Sindi na Koplo Fideli walikaribia kulinasa; lakini jitu kama Malik Mbowe halinasiki kirahisi. Sindi alimtaka Malik aweke bastola yake chini na anyooshe mikono juu. Kwamba jambazi hilo lilifikia mwisho wake. Malik alimpuuza. “Hunipati kirahisi, Sindi,” alimwambia, papo hapo akafyatua risasi mbili, akaunyakua mkoba wake. Alipoanza kutimua mbio, Inspekta Sindi aliinua bastola yake akafyatua risasi moja tu. Wote wawili, Inspekta Sindi na Koplo Fideli, walimwona akiangukia bondeni huku mkono wake ukishikilia bega lililojeruhiwa vibaya. Alipiga kelele nyingi za maumivu. Hawakumwona tena! Ni baada ya askari hao wawili kufika nyumbani kwa Perino na kushuhudia yaliyotokea ndipo Sindi alipoamua yasambazwe matangazo nchini nzima na picha yake, kwamba yeyote atakayemwona jambazi huyo, popote pale, ammalize japokuwa alikuwa na uhakika kuwa Malik asingeweza kutoka mle bondeni hai. Alikosea sana! Malik alikuwa na roho ngumu kama ya paka. Japo alijeruhiwa vibaya lakini alipona. Na balaa alilozusha huko alikokwenda halisemeki! Sasa endelea…

1 Faili
TZS 7,000
Angalia Maelezo